Nenda kwa yaliyomo

Mitazamo ya Kiyahudi juu ya Yesu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Image
Johann von Armssheim (1483) alivyochora mabishano kati ya wataalamu Wakristo na Wayahudi.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Yesu
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho   Utoto wa Yesu   Ubatizo   Arusi ya Kana   Utume wa Yesu   Mifano ya Yesu   Miujiza ya Yesu   Kugeuka sura   Karamu ya mwisho   Msalaba wa Yesu   Maneno saba   Kifo cha Yesu   Ufufuko wa Yesu   Kupaa mbinguni   Ujio wa pili  Yesu na matabiri ya Agano la Kale   Injili   Majina ya Yesu katika Agano Jipya   Yesu kadiri ya historia   Tarehe za maisha ya Yesu   Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi   Kiaramu   Bikira Maria   Yosefu (mume wa Maria)   Familia takatifu   Ukoo wa Yesu   Ndugu wa Yesu   Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya  · Mitazamo ya Kikristo   Mitazamo ya Kiyahudi   Mitazamo ya Kiislamu   Yesu katika sanaa

Mitazamo ya Kiyahudi juu ya Yesu ni ya aina mbalimbali, lakini yote haimkubali, la sivyo ingewabidi wahusika wamuamini na kubatizwa badala ya kuendelea na dini yao ambayo viongozi wake walimhukumu ni kafiri anayestahili kuuawa.

Kwa kawaida Wayahudi wanamuona Yesu kama mmojawapo kati ya wengi waliojinadi kuwa Masiya katika nyakati mbalimbali za historia ya taifa lao.[1]

Yesu anatazamwa kama yule aliyefaulu zaidi kukubalika, na kwa sababu hiyo, kuleta madhara makubwa kuliko wote.[2]

Uyahudi haujawahi kumkubali rasmi Masiya yeyote kuwa ametimiza utabiri wa manabii. Zaidi ya hayo, unaona ibada ya Wakristo kwa Yesu kuwa kinyume cha imani katika Mungu mmoja tu.[3]

Katika Karne za Kati, Judah Halevi na Maimonide walimuona Yesu (kama vile Muhammad) kama mtu muhimu katika kuandaa mataifa yote kwa ujio wa Masiya atakayeyafanya yamuabudu Mungu pekee.

Siku hizi kuna wataalamu Wayahudi wanaosema Yesu alikuwa jirani na dini yao kuliko Injili zinavyoonyesha. Mtazamo huo ulianzishwa katika karne ya 18 na Jacob Emden na Moses Mendelssohn.

Image Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mitazamo ya Kiyahudi juu ya Yesu kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
  1. Jesus of Nazareth
  2. Maimonides. Mishneh Torah, Sefer Shofetim, Melachim uMilchamot, Chapter 11, Halacha 4. Chabad translation by Eliyahu Touge.
  3. Devarim (Deuteronomy) 6:4